Friday, December 4, 2015

NISHA`S FILM PRODUCTION WAJA KIVINGINE

Ile kampuni inayoongoza kufanya vizuri upande wa filamu yaja kiaina yake. Nisha`s Film Production imeamuakuchukua kundi kubwa la wasanii wachanga na kuwapa nafasi kubwa kwa ajili ya kuonyesha uwezo wao na pamoja kutimiza lengo la kampuni hiyo ya kuwanyanyua wasanii hao wenye ndoto za kuwa mastar wakubwa ndani na nje ya nchi yao ya Tanzania. Wasanii hao nao hawakulaza damu waliweza kuonyesha uwezo wao mpaka kuwa sawa na wale mastar hivyo kuwa vigumu kuwatambua kama ndio kwanza wanaanza Game hiyo.       MZIGO MPYA SOON UTAINGIA MTAANI


Kwa taarifa zaidi mfollow Production Manager wa Nisha`s film @ochu_255

Wednesday, July 15, 2015

NISHA AMEJIOA MWENYEWE , WABONGO WASHIKWA NA BUTWAA

Usipo staajabu ya Mussa utayaona ya Farao...  huo ni msemo ambao umejitokeza katika vinywa vya watu huku wakibaki mdomo wazi baada ya kushuhudia Mwanadada NISHA (SALMA JABU) Akitoa kali ya mwaka...
Msanii wa Comedy ambae anakadiriwa kua ni wapekee wa kike Africa Mashariki ikiwemo Kenya Uganda na Tanzania katika nyanja a uchekeshaji..... Akiwa nchini China nchi iliyogubikwa na Teknolojia ya hali ya juu... NISHA alitangaza kua ameamua kujioa yeye mwenyewe... huku Aina hiyo ya ndoa ikiwa na Sitntojua kua ni ya kabila gani na kwanini aliamua kuichagua China kua ndio sehemu pekee ya kutekeleza jambo hilo....huku akivaa mavazi nusu nusu... aina hii inatambulika kama (Shemale) duniani.. huenda akawa msanii na mtu wa kwanza kufanya tukio hili la pekee nchini...
Tukirudi katika maadili ya nchi Tunagundua kua aina hii si moja kati ya zile ambazo zimekatazwa kwani ameamua kujimiliki mwenyewe..bila kuvunja sheria...za maadili ya nchi.
Hivyo sheria ya nchi haiwezi kumtuhumu kama wanavyotuhumiwa wasanii wanapovunja maadili ya nchi huko ughaibuni.
AWA GUMZO CHINA
Msanii NISHA amekua akiwaacha wananchi wa jamii ya CHINA meno nje hasa anapokwenda katika moja ya hotel nchini humo kwa lengo la kujipatia milo ya mchana.asubuhi ama usiku.. kwani amekua akiagiza vyakula vya aina ya nchi hiyo na hujitahidi kula kama amezaliwa huko.
Muonekano na kuongea kwake kuliwachekesha sana Wachina katika mitaa ya Nchini humo hasa alipokua katika mizunguko... huku akizidi kuchana shavu baada ya kupokea mialiko katika sehemu mbali mbali muhimu...ikiwa hasa ni kuiongelea sanaa ya Tanzania...na ubora wake..
AJIFUNZA
Fursa ya mwanadada NISHA kutembelea katika uwanda wa nchi hizo... Alionekana kujifunza mengi sana hasa swala la sanaa na Mazoezi.. kitu ambacho wasanii wa China wamekua wakiweka kipa umbele sana.. tofauti na Tanzania.. wasanii wanaona sanaa na mazoezi ya mwili ni vitu viwili tofauti.
Blog hii ilijaribu.. kumtafuta mwanadada NISHA kwa mazungumzo ila bila mafanikio.. kwani amekua akizongwa na shuhuli zilizompeleka huko za kisanaa....
AWA TISHIO
Safari ya NISHA na uwepo wa huko China kuna weza kua Tishio kwa wasanii wa Bongo kwani huenda akaendelea kuliteka soko la filum  Bongo kwa kile kinachodaiwa huenda  akaanguka mikataba na ma kampuni makubwa ya utoaji Filum za huko China.
KILA LA HERI SALMA JABU NISHA...




Wednesday, June 24, 2015

KOMEDI KUMPELEKA NISHA UGHAIBUNI

Sikutaka kusema mapema ila wameniwahi,..
😢tukijaaliwa na ahsante M'Mungu we ni mwema sana... Kikubwa ahsanteni sana mashabiki zangu wote,nyi ndo mnaotenda haya.
Management yng yote ahsante...
#MTAAKWAMTAA ahsante 😢😭dah
Nisha punguza comedy haikufai.. guyz kwny ugali usichague kikubwa kiwe halali ☆☆☆☆☆☆☆☆☆☆☆☆☆☆☆☆☆☆

Monday, June 1, 2015

WABUNGE NA MAWAZIRI WAISIFIA MTAA KWA MTAA

Baada ya kuona Mastar wakiisifia MTAA KWA MTAA sasa Nisha apata msg kutoka kwa wabunge pamoja na mawaziri wakimpongeza kwa kazi nzuri aliyoifanya ndani ya MTAA KWA MTAA. Ndani ya hiyo movie kuna mastar nao waliofanya yao kati ya mastar hao ni Asha Boko,Hemed Suleiman,Diana Kimary,Tausi Mdegela pamoja na mtoto wake Salma Jabu Nisha ambaye ameonyesha uwezo mkubwa anajulikana kama Iptysam Othman. Kama ilivyo kawaida ya Nisha's film huwa haiwachi wasanii wachanga nao wakafanya yao humo.


Sunday, May 31, 2015

WASANII WACHANGA WAONYESHA UWEZO WAO NDANI YA MTAA KWA MTAA

Kama ilivyokawaida ya Nisha's film production huwa haiwaachi wasanii wachanga basi humo kwenye MTAA KWA MTAA wamefanya yao. Katika kitu ambacho hakikutegemewa ni wasanii hao wachanga kuonyesha uwezo wao wahali ya juu mpaka mtu ushindwe kutambua kama kweli hawa ndio mara yao ya kwanza au ni wakongwe katika sanaa. Kama huja nunua Dvd ya MTAA KWA MTAA kanunue sasa ili uweze kujionea uwezo wa wasanii hao wachanga katika sanaa ya uigizaji. Nisha's film production lengo lake kubwa ni kuwainua wasanii wa changa hivyo huwapa nafasi za kucheza katika movie zinazotoka Nisha's film zam kwa zam. Kama na wewe ni msanii mchanga na unahitaji kushiriki katika movie za Nisha's film basi fanya ku follow page zetu za instagram ambazo ni @nishabebee @nishasfilmproduction @ochu_255 na kwa wale waliopo facebook unaweza ku join katika group letu ambalo ni Team nisha films production au unaweza kulike page yetu Nisha's film production pia kama upo whatsapp unaweza kuwasiliana na Production manager wa Nisha's film bwana Othman kwa no 0789 586057.











Saturday, May 30, 2015

MASTAR WAIPOKEA MTAA KWA MTAA KWA KISHINDO


MTAA KWA MTAA ya pokelewa kwa kishindo na mastar katika movie zilizokubaliawa na mastar basi MTAA KWA MTAA ndio movie namba moja iliyo kubalika kwani kila mmoja aliisifia na wengine kuahidi kuitafuta maana kuanzia wasanii,ma producer,ma director pamoja na wanamziki na hata wale watu wenye majina makubwa hapa nchini oda kutoka nchi mbalimbali za zidi kumiminika. Kenya,Rwanda,Burundi,Congo pamoja na nchi za bara la ulaya wanapiga simu nakuulizia ni jinsi gani wanaweza kuipata movie ya MTAA KWA MTAA.
HONGERA SALMA JABU NISHA KWA MOVIE BORA YENYE KUELIMISHA NA KUBURUDISHA










Wednesday, May 27, 2015

NISHA ASHANGAZA MAMILION YA WATU



Msanii wa filamu mwenye jina kubwa na heshima kwa jamii Salma Jabu Nisha ashangaza watu wengi baada ya filamu yake ya MTAA KWA MTAA inayotoka kesho siku ya alhamis tarehe 28/05/2015 kuisha steps na mwakala nchi nzima kugombaniana,hivyo kuwapa kuwapa kazi tena steps intertainment kutoa nakala nyingi zaidi za filamu hiyo ya MTAA KWA MTAA ambayo  imeoneshwa kupendwa na kukubaliwa  sana na mashabiki  kabla haijatoka, imeitwa maajabu kutokana kwamba filamu za star huyo asiyekuwa na scandals,mwenye sifa uchapakazi ‘’NISHA’’ kuvunja  record kazi zake kwa mauzo na kumfanya azidi kung’ara na kutoa filamu kali kupita zote kila atoapo,filamu hiyo kali ya MTAA KWA MTAA amewashirikisha  waigizaji mahiri kama Asha book,Hemedy Suleiman,Tausi Mdegela,Diana Kimary huku motto wake Nisha Iptysam Othman akionesha kung’ara zaidi naye,MTAA KWA MTAA imekuwa kiburudisho kikubwa haswa kwa kuonekana Nisha na Asha Boko kwenye mavazi ya Kitrafic huku kila mtu akitamani kujua ndani kuna nini na imekuwaje wakali hawa kuwa katika mavazi hayo. MTAA KWA MTAA itatoka kesho tarehe 28/05/2015 Mungu ibariki Mtaa kwa Mtaa ,ibariki Nisha’s film production,wabariki wasanii wanaojituma Tanzania.

Hongera Nisha MTAA KWA MTAA itazidi kufanya maajabu na kushangaza zaidi.





Sunday, May 24, 2015

ANGALIZO KWA WAANDAAJI WA TUZO

Kwanza napenda kuwapongeza wasanii wote ambao wanafanyiwa hujuma ili washuke kisanaa lakini matokeo yake wanapambana nakuendelea kusonga mbele ninachopenda kuwaambia TUZO siyo kitu kinachokufanya uwejuu bali juhudi zako katika kazi heshima na upendo kwa kila mtu ndio TUZO muhimu katika kazi yako ya yasanaa kwani itakuongezea mashabiki na kukupa maendeleo. Baada ya kuandika hayo narudi sasa kwenye mada kuu. Kwanza kabisa napenda kuanza kwenye TUZO zilinzo anza muda kidogo ambazo ni TUZO za KILIMANJARO MUSIC AWARDAS hizi TUZO zilianza kwa kasi sana watu wengi walikuwa wakizifuatilia na kuwapigia kura wasanii wanaowapenda lakini walikuja kuboronga pale walipoenda kinyume na wapigaji kura hadi leo hii tunaona TUZO za KILIMANJARO MUSIC AWARDS zipo lakini zimepoteza mvuto kama zamani na hata wapigaji kura wamepungua sio kama zilivyoanza.  Naomba tuhamie upande wapili kwenye hizi TUZO zilizoanza ambazo nazenyewe zimeshaanza kufanya ndivyo sivyo. TUZO ZA WATU hili jina ni tata kidogo kwa maana linamaana mbili maana ya kwanza Tuzo za watu yaani kuna watu maalum wameekewa hizo TUZO ndio maana ukaambiwa TUZO ZA WATU maana ya pili ambayo ndio waisema wao nikwamba watu wanawapigia kura wasanii wanao wapenda ili wagombanie hizo tuzo ndio maana ikaitwa TUZO ZA WATU hapa staki kuongea mengi kwa maana wenyewe mejionea katika wanaogombania 99% waliokuwepo ukumbini ndio walochukua TUZO. Hayo yote tisa kumi ni kwenye TUZO zililizo tolewa jana tuzo za TANZANIA FILM AWARDS ni TUZO mliboronga kupindukia kwanza mlichemka kwenye kupangalia kugombania hizo tuzo halafu jambo jengine kubwa mlilonishangaza TUZO mmeandaa wenyewe halafu nanyie wenyewe mpokatika kugombania kisha nyienyie ndio mnashinda jamani hamjui hatakula nakipofu. MWAKIFWAMBA hapa hamjengi bali mnabomoa kwani wasanii wenyewe wataanzakuchukiana pili mtajenga matabaka ya mashabiki na hapo ndio uhasama utazidi kwa wasanii. Napia mtasababisha wasanii wasiwe wana shiriki kwenye TUZO. lamwisho ninalopenda kuwaambia waandaaji wa hizi tuzo MSANII HAPANDISHWI KWA KUPEWA TUZO BALI MSANII ANAPANDA JUU KWA KAZI NZURI NA BORA.



Friday, May 22, 2015

NISHA'S FILM SOKONI TENA

Kampuni ya Nisha's Film Production yatarajia kuingiza sokoni movie yao mpya inayo julikana kama MTAA KWA MTAA akiongea hayo Bwana Othman Thiney ambaye ni Production Manager wa Nisha's Film Bwana Othman amesema MTAA KWA MTAA ni Movie nzuri ambayo Story yake haijawahi kuchezwa hapa Bongo anacho waomba watu wanunue cd original ili kuendeleza sanaa ya hapa nyumbani. MTAA KWA MTAA INATOKA MWISHO WA MWEZI HUU