Usipo staajabu ya Mussa utayaona ya Farao... huo ni msemo
ambao umejitokeza katika vinywa vya watu huku wakibaki mdomo wazi baada
ya kushuhudia Mwanadada NISHA (SALMA JABU) Akitoa kali ya mwaka...
Msanii wa Comedy ambae anakadiriwa kua ni wapekee wa kike Africa
Mashariki ikiwemo Kenya Uganda na Tanzania katika nyanja a
uchekeshaji..... Akiwa nchini China nchi iliyogubikwa na Teknolojia ya
hali ya juu... NISHA alitangaza kua ameamua kujioa yeye mwenyewe... huku
Aina hiyo ya ndoa ikiwa na Sitntojua kua ni ya kabila gani na kwanini
aliamua kuichagua China kua ndio sehemu pekee ya kutekeleza jambo
hilo....huku akivaa mavazi nusu nusu... aina hii inatambulika kama
(Shemale) duniani.. huenda akawa msanii na mtu wa kwanza kufanya tukio
hili la pekee nchini...
Tukirudi katika maadili ya nchi Tunagundua kua aina hii si moja kati ya
zile ambazo zimekatazwa kwani ameamua kujimiliki mwenyewe..bila kuvunja
sheria...za maadili ya nchi.
Hivyo sheria ya nchi haiwezi kumtuhumu kama wanavyotuhumiwa wasanii wanapovunja maadili ya nchi huko ughaibuni.
AWA GUMZO CHINA
Msanii NISHA amekua akiwaacha wananchi wa jamii ya CHINA meno nje hasa
anapokwenda katika moja ya hotel nchini humo kwa lengo la kujipatia milo
ya mchana.asubuhi ama usiku.. kwani amekua akiagiza vyakula vya aina ya
nchi hiyo na hujitahidi kula kama amezaliwa huko.
Muonekano na kuongea kwake kuliwachekesha sana Wachina katika mitaa ya
Nchini humo hasa alipokua katika mizunguko... huku akizidi kuchana shavu
baada ya kupokea mialiko katika sehemu mbali mbali muhimu...ikiwa hasa
ni kuiongelea sanaa ya Tanzania...na ubora wake..
AJIFUNZA
Fursa ya mwanadada NISHA kutembelea katika uwanda wa nchi hizo...
Alionekana kujifunza mengi sana hasa swala la sanaa na Mazoezi.. kitu
ambacho wasanii wa China wamekua wakiweka kipa umbele sana.. tofauti na
Tanzania.. wasanii wanaona sanaa na mazoezi ya mwili ni vitu viwili
tofauti.
Blog hii ilijaribu.. kumtafuta mwanadada NISHA kwa mazungumzo ila bila
mafanikio.. kwani amekua akizongwa na shuhuli zilizompeleka huko za
kisanaa....
AWA TISHIO
Safari ya NISHA na uwepo wa huko China kuna weza kua Tishio kwa wasanii
wa Bongo kwani huenda akaendelea kuliteka soko la filum Bongo kwa kile
kinachodaiwa huenda akaanguka mikataba na ma kampuni makubwa ya utoaji
Filum za huko China.
KILA LA HERI SALMA JABU NISHA...